Psalms 112
Baraka Za Mwenye Haki
1 ▼
▼ Zaburi hii imetungwa kila mstari ukianzia na herufi ya alfabeti ya Kiebrania zikifuatana tangu Aleph (A) hadi Taw (T); zote ni 22.
bMsifuni Bwana.Heri mtu yule amchaye Bwana,
mtu yule apendezwaye sana na amri zake.
2 cWatoto wake watakuwa wenye uwezo katika nchi,
kizazi cha watu waadilifu kitabarikiwa.
3 dNyumbani mwake kuna mali na utajiri,
haki yake hudumu milele.
4 eHata gizani nuru humzukia mtu mwadilifu,
yule mwenye rehema, huruma na haki.
5 fMema yatamjia mtu yule aliye mkarimu na mwenye kukopesha bila riba,
anayefanya mambo yake kwa haki.
6 gHakika hatatikisika kamwe,
mtu mwenye haki atakumbukwa milele.
7 hHataogopa habari mbaya,
moyo wake ni thabiti, ukimtegemea Bwana.
8 iMoyo wake ni salama, hatakuwa na hofu,
mwishoni ataona ushindi dhidi ya adui zake.
9 jAmetawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini;
haki yake hudumu milele;
pembe yake itatukuzwa kwa heshima.
10 kMtu mwovu ataona na kuchukizwa,
atasaga meno yake na kutoweka,
kutamani kwa mtu mwovu kutaishia patupu.
Copyright information for
SwhKC