Psalms 64
Kuomba Ulinzi Dhidi Ya Maadui
(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Daudi)
1 aEe Mungu, unisikie ninapoeleza lalamiko langu,
uyahifadhi maisha yangu kutokana na vitisho vya adui.
2 bUnifiche kutokana na shauri la siri la waovu,
kutokana na zile kelele za kundi la watenda mabaya.
3 cWananoa ndimi zao kama panga
na kuelekeza maneno yao kama mishale ya kufisha.
4 dHurusha mishale kutoka kwenye mavizio kwa mtu asiye na hatia,
humrushia ghafula bila woga.
5 eKila mmoja humtia moyo mwenzake
katika mipango mibaya;
huzungumza juu ya kuficha mitego yao,
nao husema, “Ni nani ataiona?”
6 Hufanya shauri baya la dhuluma na kusema,
“Tumebuni mpango mkamilifu!”
Hakika nia na moyo wa mwanadamu vina hila.
7 Bali Mungu atawapiga kwa mishale,
nao ghafula wataangushwa.
8 fAtageuza ndimi zao wenyewe dhidi yao
na kuwaleta kwenye maangamizi;
wote wawaonao watatikisa vichwa vyao
kwa dharau.
9 gWanadamu wote wataogopa,
watatangaza kazi za Mungu
na kutafakari yale aliyoyatenda.
10 hWenye haki na wafurahi katika Bwana,
na wakimbilie kwake;
wanyofu wote wa moyo na wamsifu yeye!
Copyright information for
SwhKC