2 Corinthians 4:2-7

2 aTumekataa mambo ya siri na ya aibu, wala hatufuati njia za udanganyifu, tukichanganya Neno la Mungu na uongo. Kinyume cha hayo, tunadhihirisha kweli waziwazi na kujitambulisha wenyewe kwenye dhamiri ya kila mtu mbele za Mungu. 3 bHata nayo Injili yetu kama imetiwa utaji, ni kwa wale tu wanaopotea. 4 cKwa habari yao, mungu wa dunia hii amepofusha akili za wasioamini, ili wasione nuru ya Injili ya utukufu wa Al-Masihi, aliye sura ya Mungu. 5 dKwa maana hatujihubiri sisi wenyewe ila tunamhubiri Isa Al-Masihi kuwa ni Bwana na sisi ni watumishi wenu kwa ajili ya Isa. 6 eKwa kuwa Mungu, yeye aliyesema, “Nuru na ing’ae gizani,” ameifanya nuru yake ing’ae mioyoni mwetu ili kutupatia nuru ya maarifa ya utukufu wa Mungu katika uso wa Al-Masihi.

7 fLakini tunayo hazina hii katika vyombo vya udongo, ili ijulikane wazi kwamba uwezo huu wa ajabu unatoka kwa Mungu wala si kwetu.
Copyright information for SwhKC