Job 3:1-6

(Ayubu 3–31)

Hotuba Ya Kwanza Ya Ayubu

Ayubu Anazungumza

1 aBaada ya jambo hili, Ayubu akafumbua kinywa chake na kuilaani siku ya kuzaliwa kwake.

2Kisha akasema:
3 b“Siku ya kuzaliwa kwangu na ipotelee mbali,
nao usiku ule iliposemekana,
‘Mtoto wa kiume amezaliwa!’

4 Siku ile na iwe giza;
Mungu juu na asiiangalie;
nayo nuru isiiangazie.

5 cGiza na kivuli kikuu kiikalie tena;
wingu na likae juu yake;
weusi na uifunike nuru yake.

6 dUsiku ule na ushikwe na giza kuu;
usihesabiwe katika siku za mwaka,
wala usihesabiwe katika siku za mwezi wowote.
Copyright information for SwhKC