Job 3:1-6
(Ayubu 3–31)
Hotuba Ya Kwanza Ya Ayubu
Ayubu Anazungumza
1 aBaada ya jambo hili, Ayubu akafumbua kinywa chake na kuilaani siku ya kuzaliwa kwake. 2Kisha akasema:3 b“Siku ya kuzaliwa kwangu na ipotelee mbali,
nao usiku ule iliposemekana,
‘Mtoto wa kiume amezaliwa!’
4 Siku ile na iwe giza;
Mungu juu na asiiangalie;
nayo nuru isiiangazie.
5 cGiza na kivuli kikuu kiikalie tena;
wingu na likae juu yake;
weusi na uifunike nuru yake.
6 dUsiku ule na ushikwe na giza kuu;
usihesabiwe katika siku za mwaka,
wala usihesabiwe katika siku za mwezi wowote.
Copyright information for
SwhKC