John 19:1-6
Isa Ahukumiwa Kusulubiwa
(Mathayo 27:15-31; Marko 15:6-20; Luka 23:13-25)
1 aNdipo Pilato akamtoa Isa akaamuru apigwe mijeledi. 2Askari wakasokota taji ya miiba, wakamvika Isa kichwani. Wakamvalisha joho la zambarau. 3 bWakawa wanapanda pale alipo tena na tena, wakisema, “Salamu! Mfalme wa Wayahudi!” Huku wakimpiga makofi usoni. 4 cPilato akatoka tena nje akawaambia wale waliokusanyika, “Tazameni, namkabidhi Isa kwenu kuwajulisha kwamba mimi sikumwona ana hatia.” 5 dKwa hiyo Isa akatoka nje akiwa amevaa ile taji ya miiba na lile vazi la zambarau. Pilato akawaambia, “Tazameni, huyu hapa huyo mtu!” 6 eWale viongozi wa makuhani na maafisa walipomwona, wakapiga kelele wakisema, “Msulubishe! Msulubishe!” Pilato akawaambia, “Mchukueni ninyi mkamsulubishe, mimi sioni hatia juu yake.”
Copyright information for
SwhKC