Psalms 64:2-7
2 aUnifiche kutokana na shauri la siri la waovu,
kutokana na zile kelele za kundi la watenda mabaya.
3 bWananoa ndimi zao kama panga
na kuelekeza maneno yao kama mishale ya kufisha.
4 cHurusha mishale kutoka kwenye mavizio kwa mtu asiye na hatia,
humrushia ghafula bila woga.
5 dKila mmoja humtia moyo mwenzake
katika mipango mibaya;
huzungumza juu ya kuficha mitego yao,
nao husema, “Ni nani ataiona?”
6 Hufanya shauri baya la dhuluma na kusema,
“Tumebuni mpango mkamilifu!”
Hakika nia na moyo wa mwanadamu vina hila.
7 Bali Mungu atawapiga kwa mishale,
nao ghafula wataangushwa.
Copyright information for
SwhKC